Grace and Truth

This website is under construction !

Search in "Kiswahili":
Home -- Kiswahili -- 17-Understanding Islam -- 058 (False feeling of security)
This page in: -- Arabic? -- Bengali -- Cebuano? -- English -- French -- Hausa -- Hindi -- Igbo -- Indonesian -- KISWAHILI -- Malayalam -- Russian -- Somali -- Ukrainian? -- Yoruba?

Previous Chapter -- Next Chapter

17. Ufahamu Uislamu
SEHEMU YA NNE: FAHAMU VIKWAZO VYA KIISLAMU DHIDI YA INJILI
SURA YA KUMI: VIKWAZO VYA KIJAMII KWA WAISLAMU WANAPOTAFAKARI KUWA WAKRISTO

10.1. Hisia danganyifu za usalama


Waislamu kwa ujumla wanaamini Qur’an kuwa kitabu pekee kitakatifu kilichotunzwa, hata kama imani ya namna hii haina thibati yoyote ya Kihistoria. Kama matokeo ya imani ya namna hii, Waislamu kwa ujumla wao hawataki wala kujisikia kusoma vitabu vya imani nyingine. Hata Muislamu msomi kupindukia hawezi kusoma Biblia kwa sababu wanaamini kwamba imechafuliwa (hivyo ni kusema Maandishi yake yamebadilishwa) au imetanguliwa (ndio kusema nafasi yake imechukuliwa ufunuo wa Mungu wa baadaye kama mbadala). Kwao, Muhammad ndiye nabii wa mwisho, vitabu vya dini zote kabla ya Uislamu haviwezi kuaminika. Hata pale Muislamu anaposoma Uislamu kwa undani na kukuta mambo ya kupingana kwa kugongana na yasiyofuata mpangilio, ni bora kwao kuwa wakana Mungu kuliko kuiamini Biblia. Walishaaminishwa kwamba Uislamu ndio dini pekee na ya kweli, wanapogundua kwamba si ya kweli hawatatafuta nyingine kama Uislamu walioamini kwamba ndio dini iliyotunza usahihi zadi na ndio ya kweli inageuka ya uongo, basi hakuna kingine chochote kile kinachoweza kuaminika tena.

www.Grace-and-Truth.net

Page last modified on March 10, 2024, at 12:17 PM | powered by PmWiki (pmwiki-2.3.3)