Grace and TruthThis website is under construction ! |
|
Home Afrikaans |
Home -- Kiswahili -- 17-Understanding Islam -- 035 (The Miracle working Christ)
This page in: -- Arabic? -- Bengali -- Cebuano? -- English -- French -- Hausa -- Hindi -- Igbo -- Indonesian -- KISWAHILI -- Malayalam -- Russian -- Somali? -- Ukrainian? -- Yoruba?
Previous Chapter -- Next Chapter 17. Ufahamu Uislamu
SEHEMU YA TATU: FAHAMU KRISTO MUISLAMU
SURA YA SITA: KRISTO KATIKA UISLAMU
6.7. Kristo mtenda miujizaTumeona upekee wa Kristo katika njia nyingi tofauti katika Uislamu. Miongoni mwake ni miujiza inayohusishwa naye: “Mimi nimekujieni na ishara kutoka kwa Mola Mlezi wenu, ya kwamba nakuundieni kwa udongo kama sura ya ndege. Kisha nampuliza anakuwa ndege kwa idhini ya Mwenyezi Mungu na nawaponesha vipofu wa tangu kuzaliwa na wakoma na ninawafufua maiti kwa idhini ya Mwenyezi Mungu, na ninakuambieni mnachokila na mnachoweka akiba katika nyumba zenu. Hakika katika haya ipo ishara kwenu ikiwa ninyi ni wenye kuamini” (Qur’an 3:49)
Licha ya maneno “ kwa idhini ya Allah” aya hii inaelezea miujiza ya Kristo ambayo hakuna yoyote katika Uislamu amefanya, ikijumuisha uumbaji. Linganisha hii na hiki kinachosemwa na Qur’an juu ya Muhammad: “Na wale waliokufuru wanasema mbona hakuteremshiwa muujiza kutoka kwa Mola wake Mlezi? Hakika wewe ni muonyaji TU, na kila kaumu ina wa kuwaongoa” (Qur’an 13:7)
Wanazuoni wa Kiislamu wanatambua kwamba “ licha yeye kuwa wa mwisho na mtume mkuu wa Mungu, hakuwezeshwa kufanya miujiza inayofanana na ile ya manabii wa kabla yake wanaosemekena kuleta ujumbe wa mdomo. Muujiza wake pekee ilikuwa na ni Qur’an pekee yake” (Mohammed Asad, Message of the Qur’an). |