Previous Chapter -- Next Chapter
SURA YA TISA: VIKWAZO VYA WAKRISTO KUSHINDA WANAPOWAINJILISHA WAISLAMU
Inapokuja suala la kumtambulisha Kristo wa waislamu hakuna anayeweza kukanusha ugumu wa kazi hiyo. Wengine wamezingatia kama jambo lisilowezekana kabisa. Ingawa japo nakubaliana na ugumu wa kazi yenyewe, lakini siichukulii kama kazi isiyowezekana kwa namna yoyote ile.
Kwa ugumu wa kazi yenyewe, kuna sababu nyingi kwa ajili ya ugumu huo. Baadhi ya sababu hizi vinatokana na Mkristo mwenyewe, na hizi ndizo ambazo tutaziangazia kwanza. Katika sura zinazofuata tutaangazia hizi sababu za ugumu zinazoleta changamoto kwa Waislamu, ambazo kwa pamoja ni muhimu na zenye msaada kwa Wakristo kuwa na tahadhari nazo. Lakini kwaza na tuzingatie swali la kwa nini tunapaswa kumtambulisha Kristo kwa Waislamu.Je tuna uchaguzi, au ni jambo ambalo sisi wakristo tunaweza kulikwepa?