Previous Chapter -- Next Chapter
13.3. Mapingamizi juu ya Utatu
Pingamini la tatu ambalo tutaitazama ni pingamizi juu ya Utatu. Ingawa Waislamu wanapinga dhana ya Utatu wa Kikristo, Qur’an na Hadith zinapinga kitu tofauti kabisa. Qur’an inawashutumu Wakristo kuabudu miungu wawili Yesu na Mariamu mbali na Allah (Qur’an 5:73, 4:171). Hata Waislamu wa sasa, wanapoongelea Utatu wanadai kwamba Ukristo unafundisha kwamba Mungu ni nafsi tatu katika nafsi moja. Hivi ndivyo watetezi wa Kiislamu wanavyoiweka:
Hata hivyo kila Mkristo anajua kwamba hakuna Katekisimo yoyote ya kanisa inayosema hivyo, badala yake Wakristo wanasema Mungu ni nafsi tatu katika umoja wa “nguvu” au “Asili”. Wakristo hawajawahi kusema kwamba nafsi tatu ni nafsi moja badala yake Mmoja mwenye nafsi tatu.
Kama wanadamu hatuna haki, mamlaka, wala uwezo wa kumwmabia Mungu yeye ni nani. Hivyo tunatakiwa tu kuchukua neno la Mungu kama mamlaka yetu ya kutuambia Mungu ni nani. Katika Biblia kutoka mwanzo kabisa Mungu anadhihirishwa kama Mungu mmoja:
Fundisho hili ni la msingi sana Katika Ukristo na Biblia inasisitiza juu yake. Mtume Paulo anasema:
na
Kwa wakati huo huo Biblia haileti Moja kama moja iliyo moja tu bali moja yenye umoja. Aya katika Kumbukumbu inatumia neno Echad “אֶחָֽד”. Neno hili katika Biblia inatumika mara kwa mara kuonyesha Muunganiko kama ilivyo atika Mwanzo 2:24 “Watakuwa mwili mmoja” Mwanzo 11:6 “Kundi moja” Kutoka 36:13“ “Maskani moja”, Kutoka 23:29 “Mwaka mmoja” na kadhalika. Kuna neno lingine la Kiebrania inayomaanisha moja: yachid “יָחִיד”. Hii neno kabisa inamaanisha nambari moja kama ilivyo katika Waamuzi 11:34 “Mwanaye na wa pekee” na Mithali 4:3 “wa pekee”. Hili neno halijawahi kutumika juu ya Mungu popote pale kwenye Biblia.
Je Biblia inasema nini juu ya nafsi tatu za Mungu?