Grace and TruthThis website is under construction ! |
|
Home Afrikaans |
Home -- Kiswahili -- 17-Understanding Islam -- 051 (Lack of confidence)
This page in: -- Arabic? -- Bengali -- Cebuano? -- English -- French -- Hausa -- Hindi -- Igbo -- Indonesian -- KISWAHILI -- Malayalam -- Russian -- Somali? -- Ukrainian? -- Yoruba?
Previous Chapter -- Next Chapter 17. Ufahamu Uislamu
SEHEMU YA NNE: FAHAMU VIKWAZO VYA KIISLAMU DHIDI YA INJILI
SURA YA TISA: VIKWAZO VYA WAKRISTO KUSHINDA WANAPOWAINJILISHA WAISLAMU
9.6. Ukosefu wa KujiaminiKatika nchi nyingi leo, Wakristo wanaoiamini Biblia ni wachache sana. Katika nchi nyingi za Kiislamu, Wakristo ni chini ya 10% ya idadi ya watu. Katika mzingira mengine idadi ya Wakristo haivuki hata 1000 (Kama vile Somalia, ambapo Waamini wa Kikrsto wanatengeneza idadi ndogo sana ya 0.01% ya idadi ya watu). Hii inafanana sana na mazingira yaliyoelezwa katika kitabu cha Hesabu: “Bali wale waliopanda pamoja naye wakasema, hatuwezi kupanda tupigane na watu hawa; kwa maana wana nguvu kuliko sisi. Wakawaletea wana wa Israel habari mbaya ya ile nchi waliyoipeleleza, wakasema, ile nchi tuliyopita kati yake ili kuipelelza, ni nchi inayowala watu wanaoikaa na watu wote tuliowaona ndani yake ni watu warefu mno. Kisha tuliwaona wanefili, wana wa Anaki, waliotoka kwa hao Wanefili; tukajiona nafsi zetu kuwa kama mapanzi, nao ndivyo walivyotuona sisi.” (Hesabu 13: 31-33)
Wakristo wanajiona namna hiyo leo, Wanashughulika sana madhaifu yao wenyewe, wakisifu dhahiri nguvu za wengine. Wanachosahau ni sehemu ya kwanza ya amri kuu ya utume “Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani” (Mathayo 28:18). Kinachohitajika leo ni ufanisi wa wachache, wale ambao wanatenda kama chumvi au nuru; bila kujali uchache wa kilichopo, itabadilisha kila kitu. |