Grace and TruthThis website is under construction ! |
|
Home Afrikaans |
Home -- Kiswahili -- 17-Understanding Islam -- 090 (Accommodation and employment)
This page in: -- Arabic? -- Bengali -- Cebuano? -- English -- French -- Hausa -- Hindi -- Igbo -- Indonesian -- KISWAHILI -- Malayalam -- Russian -- Somali? -- Ukrainian? -- Yoruba?
Previous Chapter -- Next Chapter 17. Ufahamu Uislamu
SEHEMU YA SITA: FAHAMU WAONGOFU KUTOKA UISLAMU
SURA YA KUMI NA NNE: SHIDA ZA KIJAMII WANAZOKU TANA NAZO WAONGOFU WAPYA
14.6. Makazi na ajiraPunde mtu kutoka kwenye Uislamu anapokuwa Mkristo na ikajulikana na jamii wanaweza kujikuta wanapoteza kazi na wakawa na nafasi finyu sana ya kupata nyingine mpya. Waajiri wanaweza kutokutaka kujihusisha na waongofu wapya, Labda kwa ajili ya wanavyoona binafsi inafaa au kwa hofu ya mamlaka. Hivyo hivyo inaweza kuwa ngumu kwa huyo mtu kupata makazi (Wanaweza kufukuzwa kwenye makazi yao kwa wakati huo, bila shaka kama mwanzo walikuwa wanaishi na familia zao, wanaweza kulazimika kuanza kuishi wenyewe kwa mara ya kwanza). Kwa kuongezea, msaada wowote wa kifedha kutoka kwenye familia zao utasimamishwa, na watapoteza haki yoyote ya kurithi. Hivyo muongofu kwenye baadhi ya mazingira anaweza kuishia mahali pagumu sana. Kanisa bila shaka linaweza kuwa msaada mkubwa wa kimwili katika nyakati kama hizi, Labda ni kuwasaidia kupata kazi mpya, makazi, au kusaidia kwa mda sehemu ya kuishi, fedha wakati inapohitajika. Wakati ninapotaka kuwahimiza sana wewe na kanisa lako kusaidia kwa namna hii (Hata hivyo tumeamuriwa kufanya haya katika Yakobo 2:16), Lakini weka akilini na jihadhari kwa hatari ya muongofu kuwa tegemezi kwako siku zote kwa misaada kama hiyo. |