Grace and TruthThis website is under construction ! |
|
Home Afrikaans |
Home -- Kiswahili -- 17-Understanding Islam -- 041 (Christ cured the blind and the leper, and gave life to the dead)
This page in: -- Arabic? -- Bengali -- Cebuano? -- English -- French -- Hausa -- Hindi -- Igbo -- Indonesian -- KISWAHILI -- Malayalam -- Russian -- Somali? -- Ukrainian? -- Yoruba?
Previous Chapter -- Next Chapter 17. Ufahamu Uislamu
SEHEMU YA TATU: FAHAMU KRISTO MUISLAMU
SURA YA SABA: MIUJIZA YA KRISTO NDANI YA QUR’AN
7.3. Kristo aliponya vipofu, wakoma na kuwapa uhai walio kufaMiujiza hii hakuna aliehusishwa nayo katika Uislamu, zinaweza kuonekana kawaida kwa Mkristo, na kwa sababu tunajua kwamba Kristo alifanya haya mambo kama inavyoeleza Biblia, lakini ilivyo kawaida ikiwa habari hiyo hiyo imejumuishwa kwenye Qur’an,taarifa zake kwa kina au mambo yake ya msingi inakuwa tofauti. Katika habari za kufufua wafu Qur’an hailezi matukio kadhaa tunazoweza kufikiria, kama tukio la Lazaro au mtoto wa mjane wa Naini, lakini Qur’an inatuambia mambo ya tofauti yasiokuwemo kabisa kwenye biblia. Inaeleza habari ya Yesu alipokuwa mtoto mdogo akicheza na watoto wenzake, mmojawapo alimpiga mwenzake na kumuua. Mtoto alipoona mwenzake amekufa amtupa katika mapaja ya Yesu na kukimbia. Watu walipokuja wakamkuta Yesu na damu kwenye nguo zake na kijana aliyekufa karibu naye, hivyo wakadhania kwamba ndiye aliyemuua. Yesu akachukuliwa kwenda kwa hakimu ambapo alisema hamjui huyo mtoto wala aliyemua. Watu wakaksisirika na kutaka kumuua Yesu. Yesu akaagiza walete kijana aliyekufa, walipomuuliza kwa nini akasema ili kwamba amuulize nani alimuua. Walishangaa anawezaje kuongea na kijana aliyekufa, lakini hata hivyo wakamleta. Yesu akaomba na kumfufua kijana aliyekufa kisha kumuuliza nani alimuua! Kijana aliye kufa na kufufuliwa akamwambia Yesu nani alimuua kisha na kufa tena. Hadith zingine zinazosimuliwa kuhusu Kristo ingawa hazipo kenye Qur’an au hadith. Baadhi ya waandishi wa Kiislamu wanadai hadi kwamba Kristo alimfufua Shem, mwana wa Nuhu kutoka katika wafu ili kumshuhudia; hadith nyingi kama hizi hazikubaliki na wanazuoni lakini zinaaminika na Waislamu wengi sana. Ni sehemu ya hadith ambazo angeambiwa na mtumwa wake mkristo wa Kikoptiki Mariam aliyetolewa kama zawadi kwake na kiongozi wa himaya Rumi wa Misri. |