Previous Chapter -- Next Chapter
9.7. Ukosefu wa upendo kwa Waislamu
Kutokana na miaka mingi ya mateso chini ya tawala za Kiislamu, mateso ambayo Wakristo wamepitia (bado wanapitia) chini ya Uislamu, Wakristo wengi wameshindwa kujitoa na kuwapenda Waislamu. Hii ina athari mbili. Kwanza, hakuna shauku na motisha. Licha ya amri ya Yesu ya kupenda maadui zetu na kuwaombea wanatutesa (Mathayo 5:44), asili ya ubinadamu wetu mara kwa mara inadunda ndani na inatokea tu kwamba hatutaki. Waislamu hawasitahili upendo wa Mungu, ndivyo tuvyosikia ndani. Pili, Wakristo wanaweza kutangaza upendo wa Mungu ikiwa wenyewe wameshindwa kupenda? Tunawezaje kuaminiwa tunaposema tunawapenda maadui zetu wakati hatuonyeshi upendo huo? Tunachohitaji ni moyo wa Kristo ambaye alipatanisha maadui zake na Mungu (Warumi 5:10).