Home
Links
Contact
About us
Impressum
Site Map?


Afrikaans
عربي
বাংলা
Dan (Mande)
Bahasa Indones.
Cebuano
Deutsch
English-1
English-2
Español
Français
Hausa/هَوُسَا
עברית
हिन्दी
Igbo
ქართული
Kirundi
Kiswahili
മലയാളം
O‘zbek
Peul
Português
Русский
Soomaaliga
தமிழ்
తెలుగు
Türkçe
Twi
Українська
اردو
Yorùbá
中文



Home (Old)
Content (Old)


Indonesian (Old)
English (Old)
German (Old)
Russian (Old)\\

Home -- Kiswahili -- 17-Understanding Islam -- 069 (CHAPTER THIRTEEN: MUSLIM OBJECTIONS TO CHRISTIANITY)
This page in: -- Arabic? -- Bengali -- Cebuano? -- English -- French -- Hausa -- Hindi -- Igbo -- Indonesian -- KISWAHILI -- Malayalam -- Russian -- Somali? -- Ukrainian? -- Yoruba?

Previous Chapter -- Next Chapter

17. Ufahamu Uislamu
SEHEMU YA TANO: FAHAMU MAPINGAMIZI YA WAISLAMU DHIDI YA INJILI

SURA YA KUMI NA TATU: MAPINGAMIZI YA WAISLAMU DHIDI YA UKRISTO


Katika sura hii, tutalenga tofauti za kitheolojia za Kiislamu na Ukristo. Hii lazima ndio itakuwa ndefu zaidi katika sehemu hii. Na pia bado haitatoa upana kamili wa mjadala huu, lakini ni matumaini kwamba itakusadia katika matarajio ya kushughulika na baadhi ya mapingamizi ya kawaida dhidi ya ujumbe wa Ukristo.

Nyingi katika mapingamizi haya ni rahisi kushughulika nazo na zinaangukia mbali na misingi sahihi ya uchambuzi. Wakati mwingine tunahitaji kumuuliza tunayewasiliana naye kama yupo tayari kutumia njia hiyo hiyo ya kupinga kwa dini zote mbili Uislamu na Ukristo, maana kupinga kitu katika Ukristo na huku unakikubali kitu hicho hicho katika Uislamu ni kukosa msimamo wa wazi kabisa na haina mantiki (Kama vile kupinga vita vya Msalaba lakini kukubali mauaji ya watu wa Armenia, au Muhammad kuwauwa Wayahudi kule Madina). Nitajaribu kutoa majibu juu ya baadhi ya mambo ya kawaida wanayopinga Waislamu kuliko kuorodhesha baadhi ya mapingamizi ya kawaida tunayopata kutoka kwa watu wasio Wakristo, kama vile dhana ya kuto-kuwepo kwa Mungu, au kufanana kwa baadhi ya mafundisho ya Ukristo na yale ya kipagani.

Waislamu wanatakiwa kujadiliana mambo ya dini na Wakristo kwa namna ambayo imeelezwa ndani ya Qur’an:

“Wala msijadiliane na watu wa kitabu ila kwa njia iliyo nzuri kabisa, isipokuwa wale waliodhulumu miongoni mwao. Na semeni: Tumeyaamini yaliyoteremshwa kwetu na yaliyoteremshwa kwenu. Na Mungu wetu na Mungu wenu ni mmoja: Na sisi ni wenye kusilimu” (Qur’an 29:46)

Hiyo ni kusema:

  1. Wanapaswa kujadiliana kwa maneno mazuri na kwa tabia nzuri.
  2. Wanapaswa kuamini katika vitabu vilivyokuja kabla ya Muhammad.
  3. Wanapaswa kuamini kwamba wanamuabudu Mungu mmoja na Wakristo na Wayahudi na sote tunapaswa kumtii.

Kama mazungumzo yakipamba moto, basi, unatakiwa kuwakumbusha kinachofundishwa na Qur’an.

Sasa basi, mapingamizi ya Waislamu kwa ujumla yanaangukia katika mojawapo ya makundi haya, ambayo tutarudi kuyajadili.

  1. Imani juu ya Kutunzwa kwa Qur’an na kuharibiwa kwa Biblia ya asili.
  2. Changamoto juu ya uhalali wa Biblia maana wanaamini imekwisha tenguliwa (Imefutwa na kubadilishwa).
  3. Mapingamizi juu ya Utatu.
  4. Mapingamizi juu ya Kusulubiwa kwa Kristo.
  5. Madai ya Unabii juu ya Muhammad katika Biblia.

www.Grace-and-Truth.net

Page last modified on March 11, 2024, at 01:02 AM | powered by PmWiki (pmwiki-2.3.3)